ELIMU YA MPIGA KURA 2020.
October 21, 2020
Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika kutelekeza majukumu yake ya kikatiba, mwaka huu 2020 inaratibu na kusimamia uendeshaji wa Uchaguzi wa Rais, Wabunge katika Jamhuri ya Muungano na Uchaguzi wa Madiwani kwa Tanzania Bara. Kupitia Kifungu cha 4C cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, inatoa Elimu kwa Mpiga Kura lakini pia imetoa vibali kwa Asasi mbalimbali kutoa Elimu kwa Mpiga Kura ambayo ni kwa ajili ya kuwaelimisha wananchi juu ya mambo ya msingi yatakowawezesha kutekeleza kwa usahihi jukumu la kupiga kura Siku ya Uchaguzi Mkuu ambayo ni siku ya Jumatano, tarehe 28 Oktoba, 2020.